Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Dili iliyokufa - 1

Muktasari:

  • Nilikuwa na tabia ya kucheza bahati nasibu. Siku moja nikashinda zawadi ya shilingi milioni kumi.

Ullikuwa mwaka 1980. Wakati huo nilikuwa bado mshamba ninayeishi kijijini. Nilikuwa ninaishi katika kijiji cha Kibanda kilichoko wilaya ya Muheza, mkoa wa Tanga.

Nilikuwa na tabia ya kucheza bahati nasibu. Siku moja nikashinda zawadi ya shilingi milioni kumi.

Ilikuwa ni zawadi kubwa sana. Zawadi hiyo kwa wakati huo ilikuwa mpaka uende ukaichukue Dar es Salaam.

Ikumbukwe wakati huo nilikuwa mgeni wa jiji hilo. Ilikuwa ndiyo mara yangu ya kwanza kufika Dar. Sikuwa na mwenyeji wala rafiki.

Nikiwa kwenye basi nilikuwa na mawazo mengi ya kujiendeleza.

Karibu safari nzima nikawa naisumbua akili kupata picha ya nyumba nitakayoijenga pale kijijini kwetu. Kila nyumba niliyofikiri niliona siyo nzuri. Na haikuwa kufikiri tu, bali nilikuwa nikizijenga nyumba hizo akilini na kisha kuzibomoa baada ya kuona hazikuwa nzuri.

Nilijiambia kabla ya kujenga itabidi niende Tanga nikaangalie majengo ya kujenga ili niige. Mawazo ya utajiri yalitawala kichwani mwangu huku nikijiona ni mwenye furaha kupita kiasi.

Tulifika Dar es Salaam saa tisa mchana na ni kwa vile wakati ule mabasi hayakuwa yakienda kasi kutokana na barabara kuwa mbovu.

Tangu tunaanza kuingia tu katika jiji hilo nilianza kuzishangaa barabara zilizokuwa na mataa pamoja na majengo makubwa ya ghorofa yaliyokuwa yanapendeza.

Ilikuwa ni mara yangu ya kwanza kuona milolongo mirefu ya magari na idadi kubwa ya watu kwenye mitaa. Wakati huo kituo cha mabasi ya Tanga kilikuwa pale Mnazi Mmoja.

Wakati tunashuka kwenye basi nikajiona nimenywea kutokana na ugeni wangu na ukubwa wa jiji hilo. Ingawa niliona sehemu ndogo tu ya jiji, lakini ilitosha kunidhihirishia kuwa jiji hilo ni kubwa.

Baada ya kushuka kwenye basi nikawa naangaza macho huku na huku kama vile nilitegemea kumuona mtu ninayemjua ili nimuulize ziliko ofisi za Shirika la Bahati Nasibu la Taifa, lakini sikuona sura yoyote ninayoifahamu.

Vile nilivyokuwa ninashangaa-shangaa, madereva wa teksi nao wakawa wananisumbua kuniitia teksi zao.

“Sitaki teksi,” neno hilo nikawa narudia kulitamka mara kwa mara. Lakini ukimwambia hivyo dereva mmoja, mwingine naye anakuuliza.

Nilipoona walikuwa wakinikera niliamua kuondoka. Kabla sijapiga hatua nilihisi kuguswa bega kwa nyuma. Mkono ulionigusa ulikuwa umeshupaa. Nikashituka na kugeuka nyuma kwa haraka.

Niliona mtu amesimama nyuma yangu akitabasamu. Zilinichukua kama nukta tatu hivi kumkumbuka. Alikuwa rafiki yangu wa kijijini kwetu, Dastan Lazaro, ambaye aliondoka kijijini takriban miaka mitano iliyopita kuja Dar na hakuwahi kurudi tena. Kwa vile miaka mingi ilipita na sikutegemea kukutana na mtu kama yeye katika jiji hilo nilikuwa nimeshamsahau.

Lakini kingine kilichonifanya nimsahau ni kuwa alibadilika. Alikuwa amenawiri na alivaa vizuri kama afisa wa serikali.

“Ni wewe Dastan au macho yangu?” nikamuuliza kwa furaha huku nikimpa mkono.

“Ni mimi mgosi. Habari za Kibanda?” akaniuliza huku akipokea mkono wangu.

“Kibanda ni kwema tu. Habari za Dar?” nikamuuliza huku nikiitupia macho jinzi aliyokuwa amevaa ambayo ilimtoa kweli kweli.

“Dar ni kama unavyoiona. Wazee hawajambo nyumbani?”

“Hawajambo. Umeshapata kazi nini?” dukuduku likanifanya nimuulize.

“Mwenzako ni afisa biashara kiwanda cha bia!”

“Wacha mgosi!”

“Nakuwambia kweli. Nilipokuja Dar mjomba wangu aliniendeleza kielimu. Nilisoma hadi chuo kikuu.”

“Wacha mgosi! Sasa mbona hufiki kijijini kwetu?”

“Sijapata nafasi. Kazi ni nyingi lakini mwezi ujao nachukua likizo. Nitakuja mgosi.”

“Sasa unaishi wapi?”

“Nimejenga nyumba yangu huko Buguruni na nyingine ninaimalizia sasa, iko Kigamboni.”

“Mgosi sasa wewe si wa kuchezea!”

“Kawaida tu mgosi. Umefuata nini huku Dar?” akaniuliza.

Laiti ningejua nini kingenitokea nisingemjibu kitu. Ningeachana naye na kwenda zangu.

“Nimekuja kumuona shemeji yangu mmoja, anafanyakazi Shirika la Bahati Nasibu. Unaweza kujua ofisi zao ziko wapi?”

“Nikikuelekeza hutaelewa. Labda nikupeleke mgosi.”

“Oh! Itakuwa vyema sana.”

“Twende zetu.”

Nikafuatana na Dastan huku tunazungumza. Tukaelekea Barabara ya Lumumba. Baada ya kupiga kipande cha mwendo tulitokea katika jengo moja la ghorofa ambalo liliwekewa bango lililoandikwa: Shirika la Bahati Nasibu la Taifa.

“Ni hapa mgosi,” Dastan akaniambia.

“Nashukuru sana.”

“Sasa unategemea kurudi lini Muheza?”

“Nategemea kuondoka kesho mchana.”

“Kesho mchana nitakuwa kazini. Hatutaweza kuonana. Kwa hiyo mgosi ukirudi utanisalimia wazee na washikaji wote wa Kibanda,” Dastan akaniambia kisha tukaagana. Akaenda zake.

Nilipoingia katika ofisi za shirika hilo na kujitambulisha nilikutanishwa na afisa mmoja ambaye baada ya kuiangalia kadi yangu ya bahati nasibu, aliniuliza, “Ni yako mwenyewe?”

Nikamjibu, “Ndiyo.”

“Hongera sana. Unatokea wapi?”

“Muheza.”

“Oh! Unatoka Muheza mkoani Tanga? Unatoka katika mkoa wangu. Mimi ni mwenyeji wa Korogwe. Nimefurahi kupata mshindi wa milioni kumi kutoka kwetu.”

“Kumbe wewe ni mwenyeji wa Korogwe?”

“Mimi ni Msambaa wa Korogwe. Jina lako nani?” afisa huyo akaniuliza.

Nilimtajia jina langu, akaandika kwenye karatasi kisha akaniuliza tena.

“Una umri gani?”

“Miaka 28.”

“Unafanya kazi gani?”

“Mimi ni mkulima.”

“Oh! Ukipata pesa zako utakwenda kununua trekta bila shaka.”

“Hapana. Nataka kufanya biashara.”

“Biashara gani?”

“Kununua mazao vijijini na kuyaleta hapa Dar.”

“Ni biashara nzuri lakini unatakiwa uwe mwangalifu.”

“Sasa zawadi yako tutakupatia kesho asubuhi. Una sehemu ya kulala kwa leo?”

“Hapana, sina ndugu yeyote katika jiji hili.”

“Basi tutalazimika kukupangia chumba cha hoteli ambapo utalala hadi kesho uje uchukue zawadi yako.”

“Sawa bwana.”

Baada ya hapo nikafanyiwa mpango wa kukodiwa chumba katika hoteli moja iliyokuwa katika Barabara ya Lumumba. Nakumbuka hoteli yenyewe ilikuwa inaitwa Amani Hotel.

Kama ilivyokuwa mara yangu ya kwanza kufika katika jiji hilo, ilikuwa pia mara yangu ya kwanza kulala katika chumba cha hoteli.

Haikuwa hoteli yenye hadhi kubwa lakini kwangu mimi mshamba wa Kibanda niliiona ni hoteli ya maana sana.

Asubuhi kulipokucha nilioga nikavaa nguo zangu zilezile za siku iliyopita. Nikapata chai nzuri kabla ya kuondoka hapo hotelini kwenda katika ofisi ya Shirika la Bahati Nasibu la Taifa.

Nilipofika nilikaribishwa vizuri na kuambiwa nisubiri. Kumbe walikuwa wameandaa kijisherehe cha kunikabidhi zawadi yangu. Kabla ya kijisherehe hicho kuanza niliitwa ofisini kwa yule afisa niliyezungumza naye siku iliyopita. Akaniambia,

“Tutakulipa kwa hundi ambayo utaenda kuiingiza benki. Kwa hiyo nilitaka kujua hundi yako iandikwe jina gani?”

Nikamtajia jina langu. Akaliandika kwenye kitabu. Wakati anaandika mawazo yalikuwa yanapita kichwani mwangu. Kimsingi dhamira yangu kubwa ilikuwa ni kupata pesa taslimu ili ninunue vitu nilivyokuwa nahitaji kununua. Kauli ya afisa huyo kuniambia nitalipwa kwa hundi ilikuwa kinyume na matarajio yangu.

Mimi sikuwa na akaunti benki, wakinipa hundi itaniletea usumbufu.

“Nilikuwa na ombi, afisa wangu,” nikamwambia yule afisa baada ya kuandika jina langu.

“Matarajio yangu yalikuwa ni kupata fedha taslimu kwa sababu kama nilivyokuambia jana ninahitaji kwenda kununua mazao kwa ajili ya biashara na isitoshe kulikuwa na vitu nahitaji kununua hapa Dar es Salaam. Na pia nipate pesa ya nauli. Sasa ukinipa hundi utanikwamisha.”

“Kutoa hundi kwa malipo ndiyo utaratibu wetu. Sisi hapa hatuna pesa, isipokuwa naweza kukusaidia kukuandikia hundi ya wazi ili ukienda benki ulipwe pesa zako.”

“Itakuwa afadhali.”

“Lakini si kitu kizuri kushika mkononi kiasi kikubwa cha pesa kama hicho.”

“Ni kwa dharura. Nahitaji fedha za kulipa wakulima watakaoniuzia mazao yao. Vilevile nahitaji pesa za kununua vitu hapa Dar es Salaam pamoja na pesa ya nauli.”

“Sawa, lakini kuwa makini.”

  “Nitakuwa makini.”


Nikafuatana na Dastan huku tunazungumza. Tukaelekea Barabara ya Lumumba. Baada ya kupiga kipande cha mwendo tulitokea katika jengo moja la ghorofa ambalo liliwekewa bango lililoandikwa: Shirika la Bahati Nasibu la Taifa.