Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Aucho apishana na Azam FC

AUCHO Pict

Muktasari:

  • Jana, wakati Yanga ikishinda nyumbani kwa bao 1-0 dhidi ya Coastal Union, Aucho alilazimika kucheza mechi hiyo kwa dakika 45 kisha akaomba kutoka baada kusikia maumivu  na nafasi yake kuchukuliwa na Mudathir Yahya.

Kiungo wa Yanga, Khalid Aucho atakuwa nje ya uwanja kwa takriban wiki tatu baada ya kuumia nyama za paja.

Jana, wakati Yanga ikishinda nyumbani kwa bao 1-0 dhidi ya Coastal Union, Aucho alilazimika kucheza mechi hiyo kwa dakika 45 kisha akaomba kutoka baada kusikia maumivu  na nafasi yake kuchukuliwa na Mudathir Yahya.

Leo, kiungo huyo amefanyiwa vipimo ambapo imegundulika atakuwa nje kwa wiki tatu, kwa mujibu wa taarifa ambayo iliyotolewa na Klabu  ya Yanga.

Kwa Aucho kuwa nje kwa wiki tatu kunamfanya azikose mechi tatu kuanzia mchezo wa Azam utakaopigwa keshokutwa, Aprili 10.

Mechi zingine atakazozikosa ni ile ya ugenini dhidi ya Fountain Gate Aprili 20 na ya  nyumbani Yanga itakapoikaribisha Namungo ya Lindi, Mei 13.

Hata hivyo, Yanga ina watu ambao wanaweza kuziba nafasi ya Mganda huyo kwani italazimika kuwatumia Mudathir Yahya, Duke Abuya, Jonas Mkude au Aziz Adambwile.