Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Yanga Princess imejipata

Yanga P Pict

Muktasari:

  • Mwanzoni mwa msimu Yanga ilianza vibaya Ligi Kuu (WPL) kwa mfululizo wa matokeo ikianza na sare ya 1-1 na Bunda Queens, 1-1 na Alliance Girls, 2-2 na Mashujaa na kupoteza kwa bao 1-0 dhidi ya Simba.

UNAWEZA kusema Yanga Princess chini ya kocha Edna Lena ‘ Mourinho’ imeanza kujipata kutokana na muendelezo na ubora wanaouonyesha msimu huu.

Mwanzoni mwa msimu Yanga ilianza vibaya Ligi Kuu (WPL) kwa mfululizo wa matokeo ikianza na sare ya 1-1 na Bunda Queens, 1-1 na Alliance Girls, 2-2 na Mashujaa na kupoteza kwa bao 1-0 dhidi ya Simba.

Dirisha dogo ikafanya usajili kwa baadhi ya maeneo ikiwamo eneo la ushambuliaji ikimuongeza Mrwanda, Jeaninne Mukandasyenga akitokea Rayon Sports na hadi sasa kwenye mechi nne amefunga mabao matano, kiungo Aregash Kalsa kutoka C.B.E, golikipa Zubeda Mgunda na mabeki Protasia Mbunda, Diana Mnally.

Ongezeko la nyota hao kwa kiasi kikubwa limeongeza ari ya upambanaji katika kikosi hicho kinachopambania nafasi ya ubingwa.

Akizungumzia juu ya mabadiliko ya kikosi hicho, Mourinho alisifu juhudi za wachezaji kwenye kikosi hicho akitaja uzoefu wa nyota wapya.

“Ingawa watu wanaona kuna mabadiliko makubwa lakini kwangu naona bado kidogo, nafikiri wachezaji wakipata mechi nyingi mtaona ubora wao na naamini wataleta mabadiliko makubwa, “ alisema Mourinho.