Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Ngoma ngumu, mawakili waipinga rufaa ya P Diddy

DIDY Pict

Muktasari:

  • Baada ya kesi iliyotikisa majira ya kiangazi jijini New York City, majaji walimkuta Combs hana hatia katika mashtaka ya usafirishaji haramu wa kingono na uhalifu wa mtandao (racketeering), lakini wakamhukumu kwa kukiuka Sheria ya Shirikisho ya Mann kwa kusafirisha watu kuvuka mipaka ya majimbo kwa ajili ya ngono ya malipo iliyohusishwa na kile kilichoitwa “freak-offs.”

WAENDESHA mashtaka wa serikali ya shirikisho wameanza kupinga kwa nguvu rufaa ya nyota wa Hip Hop na mfanyabiashara Sean Combs 'P Didy', wakisisitiza hakuna msingi wa kisheria wa kubatilisha hukumu yake ya makosa ya ukahaba wala kifungo chake cha miaka minne jela.⁠

Baada ya kesi iliyotikisa majira ya kiangazi jijini New York City, majaji walimkuta Combs hana hatia katika mashtaka ya usafirishaji haramu wa kingono na uhalifu wa mtandao (racketeering), lakini wakamhukumu kwa kukiuka Sheria ya Shirikisho ya Mann kwa kusafirisha watu kuvuka mipaka ya majimbo kwa ajili ya ngono ya malipo iliyohusishwa na kile kilichoitwa “freak-offs.”

Nyota huyo mwenye umri wa miaka 56 kwa sasa anatumikia adhabu yake katika gereza la shirikisho la FCI Fort Dix, huku akitarajiwa kuachiwa mwaka 2028.⁠

Katika rufaa yake, mawakili wa Combs wanadai jaji Arun Subramanian alijifanya kama “jaji wa 13” kwa kuzingatia ushahidi uliokuwa unahusu mashtaka aliyokuwa ameondolewa hatiani, ikiwemo madai yanayomhusu Cassie Ventura, wakati wa kupanga adhabu.⁠

Hata hivyo, katika majibu ya kurasa 83 yaliyowasilishwa Ijumaa (Februari 20), waendesha mashtaka wamesema jaji alifuata kikamilifu misingi ya muda mrefu ya kisheria. Wakirejea mwongozo wa Mahakama ya Juu, walisisitiza kuwa mahakama za utoaji adhabu zinaruhusiwa kuzingatia “mwenendo uliopata kuondolewa hatiani” wakati wa kupima uzito wa adhabu.⁠

“Combs anatafuta kanuni ambayo haijawahi kuwepo,” waendesha mashtaka waliandika, wakionya kiwango hicho kingewanyang’anya majaji mamlaka ya kufanya maamuzi na kuwalazimisha kupuuza mwenendo muhimu uliowasilishwa mahakamani.