Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Sichone aumaliza msimu mapema

SICHONE Pict

Muktasari:

  • Kinda huyo (17) ukiwa msimu wake wa kwanza kukitumikia kikosi hicho amecheza mechi 18 akifunga mabao sita na kutoa asisti nane.

MSHAMBULIAJI wa Trident FC inayoshiriki Ligi Daraja la Kwanza nchini Zambia, Mourice Sichone amesema kwa asilimia kubwa malengo aliyojiwekea msimu huu yametimia.

Kinda huyo (17) ukiwa msimu wake wa kwanza kukitumikia kikosi hicho amecheza mechi 18 akifunga mabao sita na kutoa asisti nane.

Akizungumza na Mwanaspoti, Sichone alisema ingawa Ligi hiyo haijatamatika lakini anahesabu amemaliza msimu kutokana na malengo aliyojiwekea ya kufunga angalau mabao matano.

Aliongeza kuwa kasi hiyo imempa mizuka ya kujiwekea msimu ujao kufunga angalau mabao 10 kuvuka malengo ya msimu uliopita.

“Sijajua kama nitaendelea kuichezea Trident kutokana na ofa nilizonazo, kwangu nimemaliza msimu nataka ujao nifunge walau mabao 10 tu,” alisema Sichone.

Hata hivyo, alisema matamanio yake makubwa kwa msimu ujao ni kuitwa kwenye kikosi cha timu ya taifa ‘Taifa Stars’.