Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

VIDEO: Soka lambeba beki Yanga, apandishwa cheo KMKM

Muktasari:

  • “Sina budi kushukuru kikosi changu kwa kuweza kunisapoti kwa kila hatua. Nitaendelea kuipambania nchi yangu," amesema Sajenti Ibrahim Bacca ambaye wazazi wake pia ni askari.

Kikosi Maalumu cha Kuzuia Magendo Zanzibar (KMKM), kimempandisha cheo nyota wa timu ya Yanga SC, Ibrahim Hamad “Ibra Bacca” kutoka Koplo na kuwa Sajenti kutokana na kuonesha kiwango bora kwenye mchezo wa soka.

“Sina budi kushukuru kikosi changu kwa kuweza kunisapoti kwa kila hatua. Nitaendelea kuipambania nchi yangu," amesema Sajenti Ibrahim Bacca ambaye wazazi wake pia ni askari.

KMKM iliyomwachia Bacca kuitumikia Yanga, ni kikosi cha ulinzi cha Zanzibar ambacho kina jukumu la kulinda mipaka ya bahari dhidi ya magendo, uvuvi haramu, na vitendo vingine vya kihalifu. Pia, KMKM husaidia katika operesheni za uokoaji baharini na usalama wa majini.