Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Liverpool, Barcelona mguu sawa kwa Jonathan Tah

TETESI Pict

Muktasari:

  • Mabosi wa Barcelona hawana wasiwasi juu ya supastaa huyo kwa sababu mwenyewe ameshaonyesha nia ya kutaka kujiunga nayo mara baada ya mkataba wake kumalizika.

BARCELONA hawana wasiwasi kuhusu mpango wa  kutaka kumsajili beki wa Bayer Leverkusen na timu ya taifa ya Ujerumani, Jonathan Tah, mwenye miaka 29, ambaye mkataba wake na vigogo hao wa  Bundesliga unatarajiwa kumalizika ifikapo mwishoni mwa msimu huu.

Mabosi wa Barcelona hawana wasiwasi juu ya supastaa huyo kwa sababu mwenyewe ameshaonyesha nia ya kutaka kujiunga nayo mara baada ya mkataba wake kumalizika.

Tah ambaye awali alionekana kuwa na nafasi kubwa ya kutua Bayern Munich, anadaiwa kutaka kujiunga na timu ya nje ya Ujerumani ambapo mbali ya Barca, kumekuwa na ripoti za kuhitajika katika kikosi cha Majogoo wa Anfield, Liverpool ambao wanatarajiwa kuingia sokoni kuongeza nguvu ya mastaa wapya dirisha lijalo.

Hata hivyo, beki huyo ameonyesha nia ya kutaka kuichezea Barcelona akiamini atapata mafanikio makubwa zaidi.


Jesus Rodriguez

REAL Betis wanahitaji Pauni 35 milioni ili kumuuza winga anayekuja juu kwa kasi Mhispania Jesus Rodriguez mwenye umri wa miaka 19, ambaye mkataba wake unatarajiwa kumalizika 2029. Rodriguez ni mmoja kati ya mastaa tegemeo katika kikosi cha kwanza cha Betis na msimu huu amecheza mechi 35 za michuano yote na akafunga mabao manne.


Aaron Ramsdale

WEST Ham United inataka kumsajili kipa wa Southampton na timu ya taifa ya England, Aaron Ramsdale, mwenye miaka 26, katika dirisha lijalo la majira ya kiangazi. Ramsdale ambaye ameshuka daraja na Southampton msimu huu mkataba wake unatarajiwa kumalizika ifikapo 2028, ambapo msimu huu chama lake hilo alilojiunga nalo akitokea Arsenal limeshuka daraja, hivyo anaweza kuondoka.


Dominic Calvert-Lewin

NEWCASTLE United wanajiandaa kutoa ofa  Burnley ili kuipata saini ya kipa wa timu hiyo, James Trafford, 22, na pia wanakamilisha mazungumzo ya kumsajili mshambuliaji wa Everton, Dominic Calvert-Lewin, ambaye mkataba wake unamalizika mwisho wa msimu huu. Mastaa hao wanatarajiwa kuwa wachezaji wa kwanza kusajiliwa na Newcastle katika dirisha lijalo.


Ademola Lookman

ATALANTA wanahitaji Pauni 51 milioni ili kumuuza mshambuliaji Ademola Lookman, 27, ambaye timu nyingi zinahitaji huduma yake tangu dirisha lililopita la majira ya kiangazi. Lookman ambaye aliwahi kuichezea Everton, alikuwa na mchango mkubwa msimu uliopita hususan katika michuano ya Europa ambapo Atalanta ilichukua ubingwa.


Mark Flekken

BAYER Leverkusen inamevutiwa na kiwango cha kipa wa Brentford, Mark Flekken, mwenye umri wa miaka 31, na inataka kumsajili katika dirisha lijalo la majira ya kiangazi. Taarifa  kutoka Sky Sports zinaeleza, Brentford inahitaji kiasi kisichopungua Euro 15 milioni ili kumuuza staa huyo wa kimataifa wa Uholanzi ambaye mkataba wake katika kikosi hicho unatarajiwa kumalizika 2027.


Frank Onyeka

MABOSI wa Brentford wanataka kumrudisha kiungo wa kimataifa wa Nigeria, Frank Onyeka, mwenye umri wa miaka 27, katika dirisha lijalo la majira ya kiangazi licha ya kuwepo kwa timu kibao zinazotaka kumsajili baada ya kiwango bora alichoonyesha katika kikosi cha Augsburg ambapo anacheza kwa mkopo. Mkataba Brentford  unamalizika 2027.


Alex Remiro

MKURUGENZI wa michezo wa Barcelona, Deco, ameanza mazungumzo na wawakilishi wa Real Sociedad ili kuipata saini ya kipa wa timu hiyo na Hispania, Alex Remiro, 30, dirisha lijalo la majira ya kiangazi. Barca inamwangalia kama mbadala wa  kipa wake raia wa Ujerumani, Marc-Andre ter Stegen, 32, ambaye amekuwa akisumbuliwa sana na majeraha ya mara kwa mara.