Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Man United, Ederson imeisha hiyo

Muktasari:

  • Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 atasaini mkataba wa miaka minne na United, ukiwa na kipengele cha kuongeza mwaka mmoja zaidi.

LONDON, England: Manchester United wamefikia makubaliano ya kulipa pauni35 milioni ili kumsajili kiungo wa Atalanta, Mbrazili Ederson.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 atasaini mkataba wa miaka minne na United, ukiwa na kipengele cha kuongeza mwaka mmoja zaidi.

Ederson bado hajafanyiwa vipimo vya afya, lakini vyanzo vinaeleza kuwa usajili huo unatarajiwa kukamilika mwanzoni mwa Julai kabla ya Manchester United kurejea mazoezini kujiandaa na msimu mpya.

Atakuwa usajili wa kwanza wa klabu tangu Michael Carrick ateuliwe kuwa kocha mkuu wa kudumu mwezi uliopita.

Makubaliano hayo pia yanajumuisha malipo ya nyongeza ya pauni3.9 milioni kulingana na mafanikio yatakayofikiwa.

Huu ni usajili wa kwanza kati ya uwezekano wa viungo watatu wa kati ambao Carrick anataka kuwaongeza katika kikosi chake msimu huu.

Manchester United imeweka kipaumbele kuimarisha eneo la kiungo baada ya kuondoka kwa Mbrazili mwenzake Casemiro, mwenye miaka 34, ambaye mkataba wake unamalizika mwishoni mwa mwezi huu.

Ederson, ambaye ameichezea Brazil mara tatu, alijumuishwa katika kikosi cha awali cha wachezaji 55 cha Kombe la Dunia, lakini hakufanikiwa kuingia kwenye kikosi cha mwisho kilichochaguliwa na kocha Carlo Ancelotti.

Akiwa Atalanta, Ederson ameonyesha uwezo wa kucheza nafasi mbalimbali za kiungo wa kati, akifunga mabao 16 katika mechi 180 za mashindano yote.

Chini ya ushawishi wa mmiliki mwenza Jim Ratcliffe, Manchester United imeboresha mfumo wake wa uchambuzi wa takwimu za wachezaji chini ya Michael Sansoni. Sansoni, ambaye awali alikuwa na nafasi ya juu katika timu ya Formula One ya Mercedes-AMG Petronas Formula One Team, amehusika kwa kiasi kikubwa katika kutambua wachezaji sahihi wa kusajiliwa kwa kushirikiana na mkurugenzi wa soka Jason Wilcox.

Carrick alithibitisha kuwa amekuwa akishiriki katika mikutano ya usajili tangu alipoteuliwa Januari kuwa mrithi wa muda wa Ruben Amorim.

Mbali ya nyota huyo, Man United pia inamfuatilia kiungo wa West Ham United, Mateus Fernandes, ingawa klabu hiyo ya London inataka kupata faida kubwa kutokana na mchezaji huyo wa Ureno ambaye walimsajili kutoka Southampton kwa zaidi ya pauni40 milioni msimu uliopita.

Aidha, United inamtamani pia Elliot Anderson, lakini kiungo huyo wa Nottingham Forest angependelea kujiunga na Manchester City.

Mbali na kuimarisha safu ya kiungo, Manchester United pia inatafuta mchezaji wa upande wa kushoto, huku Lewis Hall wa Newcastle United akiwa miongoni mwa wanaolengwa, pamoja na mshambuliaji wa kuongeza ushindani kwa Benjamin Sesko.

Klabu hiyo bado haijafanya uamuzi wa mwisho kuhusu makipa. Hilo linaweza kumjumuisha Radek Vitek, ambaye alikuwa na msimu bora akiwa kwa mkopo katika Bristol City, ambako alishinda tuzo zote za mchezaji bora wa mwaka za klabu hiyo.

Kipa huyo wa Czech mwenye miaka 22 aliiambia BBC Sport mwezi Aprili kuwa yuko wazi kuhusu mustakabali wake lakini anataka kucheza mara kwa mara, jambo linaloashiria kuwa huenda asirejee Old Trafford kama kipa wa akiba wa Senne Lammens.

Inaelezwa pia kuwa aliyekuwa kipa namba moja wa United, Andre Onana, ameambiwa anaweza kutafuta klabu nyingine. Hata hivyo, bado haijulikani kama kutakuwa na timu itakayoweza kukidhi mshahara wake mkubwa, hasa baada ya United kufuzu kushiriki Ligi ya Mabingwa msimu ujao.