Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Gets Program inazitaka pointi tisa WPL

GETS Pict

Muktasari:

  • Gets iko nafasi ya nane kwenye msimamo wa ligi na ilikuwa miongoni mwa timu mbili zilizoanza vibaya kwenye mechi 15 imeshinda mbili, sare nne na kupoteza tisa ikiruhusu mabao 39.

KATIKA kuhakikisha inasalia Ligi Kuu, Gets Program imeanza mipango ya kuzisaka pointi tisa zilizosalia, ingawa kocha wa timu hiyo, Aristides Ngowi amesema haitakuwa kazi rahisi.

Gets iko nafasi ya nane kwenye msimamo wa ligi na ilikuwa miongoni mwa timu mbili zilizoanza vibaya kwenye mechi 15 imeshinda mbili, sare nne na kupoteza tisa ikiruhusu mabao 39.

Akizungumzia juu ya mipango hiyo, kocha Ngowi alisema haitakuwa rahisi lakini wakishinda mechi hizo itawabakisha Ligi Kuu.

Aliongeza pointi tisa ni muhimu kwao za kufa na kupona ili kulipia mwanzo mbaya waliouanza.

"Ligi ilipofikia kuna vita ya ubingwa na sisi ambao tunawania nafasi za kubaki, tutapambana kwa kila hali kubaki hatutaki kurudi Ligi Daraja la Kwanza," alisema na kuongeza;

"Vijana wamekuwa na muendelezo wa kile nilichokuwa nawaelekeza, Gets tuna wachezaji wengi wadogo ambao hawana uzoefu, tunafikiri msimu ujao unaweza kuwa bora kama wakizoea haraka lakini kwa walipofika wanajitahidi sana."