Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Kocha Aykhan Farzukh amtabiria makubwa Mabula

MABULA Pict

Muktasari:

  • Mabula amejiunga na timu hiyo msimu huu akitokea Serbia alikokuwa na FK Spartak Subotica ya Ligi Kuu ya huko maarufu kama Serbian SuperLiga.

KOCHA Aykhan Farzukh wa timu ya Shamakhi FK anayoitumikia Mtanzania Alphonce Mabula amemtaja staa huyo kama kiungo atakayekuja kufanya makubwa kwani bado umri unamruhusu.

Mabula amejiunga na timu hiyo msimu huu akitokea Serbia alikokuwa na FK Spartak Subotica ya Ligi Kuu ya huko maarufu kama Serbian SuperLiga.

Chama hilo linashiriki Ligi Kuu ya Azerbaijan na Mabula amejiunga kwa mkataba wa miezi sita wenye kipengele cha kuongeza mwaka mmoja.

Akizungumza na chombo kimoja cha habari nchini humo, Farzukh alisema nyota huyo ana jitihada binafsi na cha zaidi anatumia miguu yote miwili kwa usahihi. 

"Ninaona kipaji kikubwa kwa Mabula, kama ataendelea hivi katika siku zijazo ninaamini atakuwa mmoja wa wachezaji bora wa kizazi hiki," alisema kocha huyo.

"Changamoto kubwa kwake hasa ni namna ya kutoa pasi za mbele na tumekuwa tukilifanyia kazi mazoezini."

Kiungo huyo wa chini hadi sasa amecheza mechi 11 tangu ajiunge na timu hiyo akifunga bao moja.