Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Luis Enrique hakutaka kazi ya PSG

ENRIQUE Pict

Muktasari:

  • Mhispania huyo, aliyeteuliwa kuwa kocha wa PSG mwezi Julai 2023, pia alishinda Ligi ya Mabingwa akiwa kocha wa Barcelona mwaka 2015.

Kocha Luis Enrique sasa amejiunga na kundi la makocha mashuhuri waliowahi kushinda Kombe la Ulaya au Ligi ya Mabingwa mara tatu: Bob Paisley, Pep Guardiola, Carlo Ancelotti na Zinedine Zidane.

Mhispania huyo, aliyeteuliwa kuwa kocha wa PSG mwezi Julai 2023, pia alishinda Ligi ya Mabingwa akiwa kocha wa Barcelona mwaka 2015.

Cha kushangaza ni kwamba mwanzoni hakutaka kuichukua kazi hiyo.

Mwandishi wa habari Guillem Balague amesema: “Alipoombwa kwanza amesema, ‘Timu yenu imejaa nyota, sina hamu.’

“Baadaye akaahidiwa kuwa angeweza kubadili utamaduni wa klabu. Swali halikuwa tena jinsi ya kushinda Ligi ya Mabingwa, bali ni aina gani ya soka walitaka kucheza.

ENR 01

“Jibu lilikuwa soka la kushambulia na kuvutia, na Luis Enrique aliona anaweza kulitekeleza hilo.”

Kuondoka kwa Mbappe kulisaidia timu kuwa imara zaidi

Chini ya Luis Enrique, PSG ilimpoteza mfungaji wake bora wa muda wote na mshindi wa mara tano wa tuzo ya Mchezaji Bora wa Ligue 1, Kylian Mbappe, ambaye alijiunga na Real Madrid bure mwaka 2024.

Hata hivyo, kuondoka kwake kunaonekana kuisaidia timu kupata uwiano bora zaidi.

Katika msimu wao wa kwanza bila Mbappe, PSG ilifunga mabao 44 zaidi katika mashindano yote ikilinganishwa na msimu wake wa mwisho klabuni.

ENR 02

“Kila mtu anacheza kama sehemu ya timu,” amesema Balague.

“PSG ndiyo timu yenye kadi chache za njano katika ligi kuu za Ulaya. Hilo linaonyesha nidhamu ya kihisia na ukweli kwamba kila mchezaji anafanya kazi kwa ajili ya mwenzake.

“Luis Enrique amesema wakati Mbappe anaondoka kuwa angependelea kuwa na wachezaji watano wanaofunga mabao 10 kila mmoja badala ya mchezaji mmoja anayefunga mabao 50.

“Msimu huu PSG imekuwa na wafungaji 20 tofauti. Huu ni mfumo wa pamoja.”

PSG pia imefikia rekodi ya mabao mengi zaidi yaliyofungwa katika msimu mmoja wa Kombe la Ulaya/Ligi ya Mabingwa, mabao 45, sawa na yale yaliyofungwa na Barcelona msimu wa 1999-2000.

Uhusiano maalum kati ya Luis Enrique na mashabiki wa PSG

Luis Enrique pia ameunda uhusiano wa kipekee na mashabiki wa PSG.

Baada ya kushinda Ligi ya Mabingwa mwaka jana, mashabiki walionyesha bendera maalum kwa heshima yake na binti yake Xana Martinez aliyefariki dunia mwaka 2019 akiwa na umri wa miaka tisa.

Bendera hiyo ilionyesha Luis Enrique na binti yake wakipandikiza bendera ya Barcelona katikati ya uwanja baada ya ushindi wa fainali dhidi ya Juventus mwaka 2015 mjini Berlin.

Katika fainali ya Budapest dhidi ya Arsenal, mashabiki wa PSG walionesha bango kubwa likimuonyesha Luis Enrique akiwa amebeba kombe la Ligi ya Mabingwa.

Baada ya mchezo, mashabiki walimshangilia kwa nguvu huku akibebwa juu na wachezaji wake akiwa ameshika kombe hilo.

Baada ya kupokea medali yake, Luis Enrique alicheza na kushangilia pamoja na rais wa PSG, Nasser Al-Khelaifi, wakifurahia taji ambalo kwa miaka mingi lilikuwa ndoto ngumu kwa klabu hiyo.

Sasa, si mara moja tena, bali mara mbili mfululizo.


MAKOCHA WA MATAJI

Carlo Ancelotti: AC Milan 2003, 2007; Real Madrid 2014, 2022, 2024

Luis Enrique: Barcelona 2015; Paris St-Germain 2025, 2026

Pep Guardiola: Barcelona 2009, 2011; Manchester City 2023

Zinedine Zidane: Real Madrid 2016, 2017, 2018

Bob Paisley: Liverpool 1977, 1978, 1981