Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

PSG ya Luis Enrique ilivyofikia kilele chake Ulaya

PSG Pict

Muktasari:

  • Kai Havertz aliipa Arsenal uongozi wa mapema, lakini Ousmane Dembele alisawazisha kwa mkwaju wa penalti katikati ya kipindi cha pili. Mchezo huo ulimalizika kwa sare hata baada ya muda wa nyongeza, kabla ya PSG kushinda katika mikwaju ya penalti iliyokuwa na ushindani mkubwa.

PARIS, UFARANSA: PSG wametawazwa mabingwa wa Ulaya kwa mara nyingine tena. Kikosi cha Luis Enrique kilihitaji mikwaju ya penalti kuishinda Arsenal, mabingwa wa Ligi Kuu England, katika fainali ya Ligi ya Mabingwa iliyochezwa Budapest Jumamosi. 

Kai Havertz aliipa Arsenal uongozi wa mapema, lakini Ousmane Dembele alisawazisha kwa mkwaju wa penalti katikati ya kipindi cha pili. Mchezo huo ulimalizika kwa sare hata baada ya muda wa nyongeza, kabla ya PSG kushinda katika mikwaju ya penalti iliyokuwa na ushindani mkubwa.

Baada ya kuichapa Inter Milan mabao 5-0 katika fainali ya mwaka uliopita, PSG wamekuwa timu ya pili katika enzi ya Ligi ya Mabingwa kutetea taji hilo, baada ya Real Madrid kushinda mataji matatu mfululizo kati ya mwaka 2016 na 2018.

Kwa ujumla, hii ni mara ya 10 katika historia ya Kombe la Ulaya kwa timu kushinda ubingwa huo mara mbili au zaidi mfululizo.

Baada ya miaka mingi ya kujaribu kufikia mafanikio ya Ulaya kwa kutegemea ubora wa nyota binafsi kama Kylian Mbappé, Lionel Messi na Neymar, ushindi huu unaonekana kuthibitisha kuwa mafanikio ya PSG yamejengwa juu ya nguvu ya pamoja ya timu nzima.

Luis Enrique ndiye aliyekuwa mbunifu mkuu wa mabadiliko hayo. Rekodi ya kocha huyo Mhispania katika fainali za Ligi ya Mabingwa bado bora na sasa ameshinda fainali zote tatu alizoongoza katika mashindano hayo baada ya kuiongoza Barcelona kutwaa ubingwa 2015 kabla ya kuiongoza PSG kushinda mataji mawili mfululizo.

Miongoni mwa makocha wote waliowahi kuongoza angalau mechi 50 za Ligi ya Mabingwa, Luis Enrique ana asilimia 63.2 ya ushindi, kiwango ambacho kiko juu zaidi kuliko wote. Hakujawa na shaka kuhusu namna PSG walivyofanikisha jambo hilo.

Ingawa hawakuwa katika kiwango bora cha kushambulia dhidi ya safu ngumu ya ulinzi ya Arsenal, walipata bao muhimu. Bao hilo lilifanya PSG kumaliza kampeni ya Ligi ya Mabingwa ya 2025-26 ikiwa imefunga mabao 45, sawa na rekodi ya mabao mengi zaidi yaliyofungwa katika msimu mmoja wa mashindano hayo.

Idadi hiyo imechangiwa na mfumo mpya wa mashindano. PSG walishindwa kumaliza katika nafasi nane za juu kwenye hatua ya ligi, jambo lililowalazimu kucheza mechi mbili za ziada dhidi ya Monaco katika hatua ya mtoano ya mchujo, na hivyo kupata nafasi zaidi za kuongeza mabao yao.

Kiini cha safu ya ushambuliaji kimekuwa Khvicha Kvaratskhelia. Ingawa hakuwa bora zaidi huko Budapest, lakini ndiye aliyesababisha penalti ambayo Dembele alifunga bao la kusawazisha, na alikuwa muhimu katika safari ya PSG kuelekea fainali.

Alionyesha kiwango cha juu dhidi ya Bayern Munich katika nusu fainali akifunga mabao mawili katika mchezo wa kwanza kabla ya kutoa pasi ya bao kwa Dembele katika mchezo wa marudiano. Michango hiyo ilimfikisha katika uhusika wa mabao 10 katika hatua za mtoano za Ligi ya Mabingwa msimu huu, akibaki bao moja kufikia rekodi ya muda wote.

Ushindi wa Budapest pia uliongeza rekodi ya PSG kutofungwa katika mechi 12 za hatua ya mtoano ya Ligi ya Mabingwa, wakishinda mechi 10 na kutoka sare mbili.

Aston Villa ndiyo timu ya mwisho kuifunga PSG katika hatua ya mtoano, iliposhinda mabao 3-2 katika Uwanja wa Villa Park kwenye robo fainali ya msimu wa 2024-25.

Hata hivyo, PSG waliendelea kusonga mbele katika hatua hiyo.
Uwezo wao wa kuziondoa timu za England umekuwa wa kipekee katika misimu ya hivi karibuni.

Kikosi cha Luis Enrique sasa kimeshinda kila moja ya hatua sita za mwisho za mtoano za Ligi ya Mabingwa dhidi ya timu za Ligi Kuu England.

Manchester City ndiyo timu ya mwisho kutoka England kuiondoa PSG, jambo lililotokea katika nusu fainali 2020-21.

Ingawa Ligi Kuu England bado inaendelea kutambuliwa kama yenye nguvu zaidi duniani kwa mujibu wa viwango vya soka duniani, mataji mawili mfululizo ya PSG Ulaya yameifanya klabu hiyo kuwa ya kiwango cha kupimia mafanikio katika soka la bara hilo.

MAKOCHA WENYE ASILIMIA BORA LIGI YA MABINGWA
Luis Enrique - 63.3% (ushindi 50 katika mechi 79)
Pep Guardiola – 61.3% (117/191)
Louis van Gaal – 60.0% (57/95)
Thomas Tuchel – 59.7% (40/67)
Zinedine Zidane – 58.5% (31/53)