Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Yanga ilivyoipiga bao Simba Ligi Kuu

DABI Pict

Muktasari:

  • Ukiangalia takwimu za duru la kwanza, kisha ukalinganisha na zile za duru la pili, utabaini Yanga imepiga hatua mbele, huku Simba ikipigwa bao katika suala zima la kukusanya pointi na kufunga mabao.

KUNA mstari mwembamba sana unaozitenganisha Yanga na Simba katika mbio za ubingwa wa Ligi Kuu Bara msimu huu. Hii inatokana na namna ambavyo timu hizo zilimaliza duru la kwanza na zilivyoanza duru la pili hadi sasa zilipofikia.

Ukiangalia takwimu za duru la kwanza, kisha ukalinganisha na zile za duru la pili, utabaini Yanga imepiga hatua mbele, huku Simba ikipigwa bao katika suala zima la kukusanya pointi na kufunga mabao.

Yanga inayopambania kutetea taji lake la Ligi Kuu Bara, ilimaliza duru la kwanza ikiwa nyuma ya Simba kwa tofauti ya pointi moja, lakini sasa yenyewe ipo kileleni kwa tofauti hiyohiyo ya pointi moja.

Simba inayosaka taji la Ligi Kuu Bara ililolikosa kwa misimu mitatu mfululizo, ilipambana duru la kwanza na kumaliza kileleni ikikusanya pointi 40 katika mechi 15 baada ya kushinda 13, sare moja na kupoteza moja.

DB 06

Wakati Simba ikimaliza kileleni, Yanga ilikuwa na pointi 39 baada ya mechi 15, ikishinda 13 sawa na Simba, lakini ikapokea vichapo viwili huku ikiwa haina sare. Kupoteza mechi mbili kwa Yanga ndiyo ilichangia wao kuzidiwa na Simba.

Kitendo cha Yanga kupoteza mechi mbili mfululizo za duru la kwanza baada ya kushuka dimbani mara 10, fasta ikaachana na Kocha Miguel Gamondi, kijiti chake kikachukuliwa na Sead Ramovic ambaye aliiongoza timu hiyo katika mechi sita za ligi na kushinda zote kabla ya kusepa akimwacha Abdihamid Moulin kusimamia mechi moja dhidi ya KenGold na kushinda kwa mabao 6-1, ndipo akaja Miloud Hamdi.

Hadi sasa katika mechi tano za ligi ambazo Hamdi ameiongoza Yanga, ameshinda nne na sare moja dhidi ya JKT Tanzania ambayo ilikuwa ya kwanza kwake kukaa benchi baada ya ile ya kwanza kuwa jukwaani akiishuhudia timu hiyo ikiichapa KenGold.

Kwa takwimu za duru la pili kulinganisha na zile za duru la kwanza, Yanga imeonekana kufanya vizuri zaidi baada ya kukusanya pointi nyingi (19) zaidi ya Simba (17) huku zote zikishuka dimbani mara saba. Katika kuzisaka pointi 21 kwenye mechi saba, Yanga imepoteza mbili na Simba ikipoteza nne.

DB 01

Wakati Yanga ikifanya mabadiliko ya benchi lake la ufundi kwa timu hiyo kunolewa na makocha watatu, Simba imeendelea kubaki na Fadlu Davids ambaye alianza msimu na kikosi hicho.

Hata hivyo, licha ya Simba kupoteza mechi moja ya ligi na kutoka sare tatu msimu huu, bado wenyewe wanasisitiza wanajenga timu kwa ajili ya baadaye ingawa moto wanaouwasha umekuwa tishio kwa wapinzani.

Mabadiliko ya Yanga yameifikisha hapo ilipo sasa kwani mbali na kukusanya pointi nyingi, pia imekuwa imara katika kufunga mabao kulinganisha na Simba.

Katika duru la kwanza, Yanga ilipocheza mechi 15, ilifunga mabao 32 ikiwa ni wastani wa kufunga mabao 2.1 kwa mechi.

Katika duru la pili, Yanga ikiwa imecheza mechi saba, imefunga mabao 26, wastani wa mabao ni 3.7 kwa mechi, ukiongezeka kwa 1.6 kutoka duru la kwanza.

DB 02

Kwa upande wa Simba, duru la kwanza ilifunga mabao 31 ikiwa ni wastani wa mabao 2.0 kwa mechi.

Duru la pili, Simba imecheza mechi saba na kufunga mabao 21 huku wastani ukiwa ni mabao matatu kwa mechi ikionyesha hakuna mabadiliko yoyote.


KINACHOWEZA KUTOKEA

Yanga na Simba kila moja imebakiwa na mechi nane ikiwemo moja itakayowakutanisha baada ya kuahirishwa Machi 8, mwaka huu. Mchezo huo unaweza kuleta taswira nyingine katika mbio za ubingwa kwani Yanga ikishinda, itaiacha Simba kwa pointi nne, lakini ikiwa tofauti, Simba itakaa juu kwa tofauti ya pointi mbili. Sare itaendelea kuwafanya kukimbizana kwa tofauti ya pointi moja.

Katika mechi nane zilizobaki, Yanga italazimika kucheza nne ugenini dhidi ya Tabora United, Azam, Fountain Gate na Tanzania Prisons, huku zingine nne nyumbani dhidi ya Simba, Coastal Union, Namungo na Dodoma Jiji. Kati ya zile za ugenini, moja pekee dhidi ya Azam haitasafiri kwenda nje ya Dar es Salaam, zilizobaki italazimika kusafiri.

Katika duru la kwanza, Yanga ilipocheza dhidi ya timu hizo, ilikusanya pointi 18 kati ya 24 kutokana na kushinda sita na kupoteza mbili huku matokeo yakiwa hivi; Simba 0-1 Yanga, Coastal Union 0-1 Yanga, Yanga 0-1 Azam, Yanga 1-3 Tabora United, Namungo FC 0-2 Yanga, Yanga 4-0 Tanzania Prisons, Dodoma Jiji 0-4 Yanga na Yanga 5-0 Fountain Gate.

DB 05

Simba kwenye mechi nane zilizobaki, nne nyumbani na nne ugenini huku hizo mechi nane moja pekee dhidi ya KenGold ndiyo itasafiri kwenda nje ya Dar kucheza, zilizobaki zote itacheza Dar es Salaam.

Mechi zilizobaki za Simba ni dhidi ya Yanga, Mashujaa, JKT Tanzania, Pamba Jiji, KMC, Singida Black Stars, KenGold na Kagera Sugar.

Katika duru la kwanza dhidi ya timu hizo, Simba ilikusanya pointi 21 kati ya 24 baada ya kushinda saba na kupoteza moja matokeo yakiwa hivi; Simba 0-1 Yanga, Mashujaa 0-1 Simba, Simba 4-0 KMC, Pamba Jiji 0-1 Simba, Simba 2-0 KenGold, Kagera Sugar 2-5 Simba, Simba 1-0 JKT Tanzania na Singida BS 0-1 Simba


MATOKEO SIMBA DURU LA KWANZA

Simba 3-0 Tabora United

Simba 4-0 Fountain Gate

Azam FC 0-2 Simba

Dodoma Jiji 0-1 Simba

Simba 2-2 Coastal Union

Simba 0-1 Yanga

TZ Prisons 0-1 Simba

Simba 3-0 Namungo

Mashujaa FC 0-1 Simba

Simba 4-0 KMC

Pamba Jiji 0-1 Simba

Simba 2-0 KenGold

Kagera Sugar 2-5 Simba

Simba 1-0 JKT Tanzania

Singida BS 0-1 Simba

DB 04

MATOKEO YANGA DURU LA KWANZA

Kagera Sugar 0-2 Yanga

KenGold 0-1 Yanga

Yanga 1-0 KMC

Yanga 4-0 Pamba Jiji

Simba 0-1 Yanga

Yanga 2-0 JKT Tanzania

Coastal Union 0-1 Yanga

Singida BS 0-1 Yanga

Yanga 0-1 Azam

Yanga 1-3 Tabora United

Namungo FC 0-2 Yanga

Yanga 3-2 Mashujaa

Yanga 4-0 TZ Prisons

Dodoma Jiji 0-4 Yanga

Yanga 5-0 Fountain Gate


MSIMAMO DURU LA KWANZA

          P       W      D      L       F       A       PTS

1. Simba     15      13      1        1        31      5        40

2. Yanga     15      13      0        2        32      6        39


DB 03

MATOKEO SIMBA DURU LA PILI

Tabora United 0-3 Simba

Fountain Gate 1-1 Simba

Simba 3-0 TZ Prisons

Namungo FC 0-3 Simba

Simba 2-2 Azam FC

Coastal Union 0-3 Simba

Simba 6-0 Dodoma Jiji


MATOKEO YANGA DURU LA PILI

Yanga 4-0 Kagera Sugar

Yanga 6-1 KenGold

JKT TZ 0-0 Yanga

KMC FC 1-6 Yanga

Yanga 2-1 Singida BS

Mashujaa FC 0-5 Yanga

Pamba FC 0-3 Yanga


MSIMAMO DURU LA PILI

          P       W      D      L       F       A       PTS

1. Yanga     7        6        1        0        26      3        19

2. Simba     7        5        2        0        21      3        17


MECHI ZILIZOBAKI SIMBA

Yanga v Simba

Simba v Mashujaa

JKT TZ v Simba

Simba v Pamba Jiji

KMC FC v Simba

Simba v Singida BS

KenGold v Simba

Simba v Kagera Sugar


MECHI ZILIZOBAKI YANGA

Yanga v Simba

Tabora United v Yanga

Yanga v Coastal Union

Azam v Yanga

Fountain Gate v Yanga

Yanga v Namungo

TZ Prisons v Yanga

Yanga v Dodoma Jiji