Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Makalla: Wanaruangwa ishikilieni Namungo FC

NAMUNGO Pict

Muktasari:

  • Kwa sasa, Namungo  inashika nafasi ya 11 kwenye msimamo wa Ligi Kuu ikiwa imecheza michezo 26 na kukusanya pointi 28.

KATIBU wa Halmashauri Kuu (NEC), Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Amos Makalla, amewahimiza wakazi wa Ruangwa mkoani Lindi kuendelea kuiunga mkono timu ya Namungo iliyopo katika Ligi Kuu Bara kwa vile  ni kichocheo kikubwa cha maendeleo ya kiuchumi wilayani humo.

Akizungumza leo Jumapili, Aprili 13, 2025, na wananchi  wilayani Ruangwa, Makalla amesema, uwepo wa timu hiyo katika Ligi Kuu ya NBC umekuwa na mchango mkubwa katika kuimarisha shughuli za kiuchumi.

“Namungo inashiriki Ligi Kuu, ina uwanja hapa. Hii maana yake ni kwamba timu zote za ligi hiyo zinakuja kucheza hapa Ruangwa zikiwamo Simba na Yanga. Hapo ndipo utalii wa kimichezo unapofanyika, hoteli zinapata wateja, mama na baba lishe wanapata wateja nawasafirishaji, hivyo uchumi unakua,” amesema Makalla.

Kwa sasa, Namungo  inashika nafasi ya 11 kwenye msimamo wa Ligi Kuu ikiwa imecheza michezo 26 na kukusanya pointi 28.