Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Wasaudia waweka mzigo kwa Greenwood

WAARABU Pict

Muktasari:

  • Greenwood alijiunga na Marseille katika dirisha la majira ya kiangazi mwaka jana  kwa mkataba wa miaka mitano akitokea Manchester United, na kwa kiasi kikubwa ameonyesha kiwango bora hadi sasa.

MARSEILLE, UFARANSA: MSHAMBULIAJI wa Marseille, Mason Greenwood huenda akatimkia Saudi Arabia katika dirisha la majira ya kiangazi baada ya matajiri hao kuweka mezani Euro 90 milioni kwa ajili ya kuipata huduma yake.

Greenwood alijiunga na Marseille katika dirisha la majira ya kiangazi mwaka jana  kwa mkataba wa miaka mitano akitokea Manchester United, na kwa kiasi kikubwa ameonyesha kiwango bora hadi sasa.

Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 23 tayari amefunga mabao 17 katika mechi 30 kwenye mashindano yote akiwa na timu hiyo ya Ligue 1, na pia ametoa asisti nne za mabao.

Hata hivyo, hivi karibuni ameingia katika sintofahamu na kocha Roberto de Zerbi ambaye ameweka wazi kwamba hafurahishwi na utendaji kazi wake na ameweka wazi kwamba anaona hajitumi inavyotakiwa.

Ikiwa usajili wake kwenda Saudi Arabia utafanikiwa kwa kiasi tajwa cha pesa kama ilivyoripotiwa na Fichajes, Man United pia itafaidika kwa kupata pesa nyingi kwani katika mkataba wa mauziano kati ya Marseille na Man United kuna kipengele kinachowapa Mashetani Wekundu asilimia 50 ya mauzo.

Hata hivyo, Greenwood mwenyewe bado anatamani kuendelea kusalia katika viunga vya Marseille licha ya nyakati ngumu anazopitia kwani anaamini anaweza kurudisha kiwango chake.