Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

TFF yamfungia Jamal Bakhresa mwaka mmoja

Muktasari:

  • “Kamati ya Nidhamu ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imemfungia Kiongozi wa Azam FC, Jamal Bakhresa kujishughulisha na mpira wa miguu kwa kipindi cha mwaka mmoja”.

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kupitia kamati yake ya nidhamu imemfungia kiongozi wa Azam FC, Jamal Bakhresa kujihusisha na mpira wa miguu kwa kipindi cha mwaka mmoja baada ya kumkuta na hatia kutokana na vitendo vya utovu wa nidhamu alivyofanya kabla na baada ya mechi ya Fainali ya Kombe la Shirikisho la CRDB iliyochezwa kisiwani Pemba.

Kupitia taarifa iliyotolewa na TFF imesema:

“Kamati ya Nidhamu ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imemfungia Kiongozi wa Azam FC, Jamal Bakhresa kujishughulisha na mpira wa miguu kwa kipindi cha mwaka mmoja”.

“Bakhresa ametiwa hatiani kutokana na vitendo vya utovu wa nidhamu alivyofanya kabla na baada ya mechi ya Fainali ya Kombe la Shirikisho la CRDB iliyochezwa kisiwani Pemba”.

“Mlalamikiwa alikiri kufanya makosa mbele ya Kamati hiyo inayoongozwa na Wakili Alex Mushumbusi kwa malalamiko yote mawili yaliyowasilishwa dhidi yake”.

“Aliomba radhi kwa TFF kwa makosa aliyofanya, na kuahidi kutorudia tena”.

“Kamati ilimtia hatiani kwa kuzingatia Ibara ya 11(f) ya Kanuni za Nidhamu za TFF, Toleo la 2021”.